Monday, August 2, 2010

Na Bwana Mungu wetu, atafuta kila chozi katika macho yetu!

Je, unadhani unayo fadhaha? Una majonzi ambayo ni kama hujui lini utapata faraja? Ni kweli wakati mwingine kuna kile tunachikiita ubinadamu katika maisha yetu. Tunazidiwa na kujikuta tunalia kwa uchungu wakati yanapotukuta yale ambayo tusingependa kukutana nayo katika maisha.


Wako watu ambao wamekata tamaa, kwao kuishi na kufa hakuna tofauti, vyote vina maana moja. Wana mambo wanayopitia wao wanasema hayaelezeki. Ndio! Nakubaliana nao, kwamba mambo hayo ni ngumu hata kuyasimulia, ndio maana kwa sababu ya kushindwa kuyasimulia, hujikuta wakibubujikwa machozi katika nyuso zao.

Hata hivyo, pamoja na kulia na kuugua kwetu, kwa wale ambao wamemwamini Kristo Yesu, wanalo tumaini, ndio wanalotumaini, ndio maana wanayo hakika kwamba mateso ya dunia hii ni ya kitambo tu, ni kweli watalia, lakini hawatalia milele, watalia kwa kitambo tu! tena kitambo kidogo sana!

Baada ya maisha haya yako maisha ambayo ni ngumu kuyaeleza katika lugha zetu za kibinadamu, namaanisha Kizungu, Kihindi, Kiswahili, Kinyakyusa, Kisukuma, Kichagga, Kimasai nk. Ni ngumu mno kueleza. Lakini kuna maisha hayo, tena yanaitwa maisha ya milele na milele, yaani yasiyo na mwisho.

Ndio maana nataka nikualike wewe ambaye unapitia chamamoto za maisha, mjie Yesu. Usije ukathubutu kuchukua uamuzi wa kujiua, kwa sababu baada ya kufa kuna maisha tena, yako ya kule Jehanam ya moto, na kuna yale ya kwenye Mji mpya Mtakatifu wa Mungu!

Kujitoa uhai sio suluhisho, maana kwa kufanya hivyo ni kukata tiketi ya kwenda kwenye adhabu ingine isiyo na mwisho, lakini unaweza ukaepuka na kuamua kumpa Kristo Yesu maisha yako, yeye atafanyika raha na faraja nafsini mwako!

0713 550 778
0762 822 093

KARIBUNI

Ninayo furaha kubwa kuwakaribisha watu wote katika blogu hii mpya ya Kikristo. Jambo moja nina hakika nalo, kwamba ziko blogu nyingi za Kiksrito ambazo umekuwa ukijengwa kwa hizo, tunachofanya sisi kwenye blogu hii ni kujiunga na Watumishi wengine ambao walianza kazi ya kufundisha na kuhubiri kwa kutumia Internet.

Tunawahakikishia kwamba kila kitu kitakwenda sawasawa na vile BWANA alivyokusudia. Ombi letu ni hili, kila wakati ambapo utakuwa umebarikiwa na huduma hii, mpe Mungu Utukufu na kisha nena waambie wengine!

Ni mimi Kiongozi wa timu nzima ya lisharoho.blogspot.com kwa niaba ya wenzangu,
Daniel R. Gingo
MUNGU AZIDI KUTUBARIKI!